John Rukono
Ni furaha yake mama, mwingi wa matumaini
Mateso yake waama, mwana nipate imani
Hakuiweka lawama, hata kiwa masikini
Furaha ya mama yangu, mwana ndiyo nilo nayo
Miezi tisa tumboni, mama liniangalia
Kwa uwezo wa Manani, mama akajifingua
Ni mdogo kwa yakini, na mambo sikuyajua
Furaha ya mama yangu, ndiyo mimi nilo nayo
Kijusi hadi kitoto, mamangu alinilea
Nikawa kama lipyoto, ila hakunichukia
Ningali bado mtoto, adabu linipatia
Furaha ya mama yangu, ndiyo mimi nilo nayo
Baba alienda zake, kumwacha mama mjane
Akalia asicheke, machozi yalo manene
Ila leo si makeke, aibu liisha tene
Furaha ya mama yangu, ndiyo mimi nilo nayo
Machozi huwa yatoka, kitaka usaindizi
Wana eti ni baraka, ila sivyo waziwazi
Mama naomba Rabuka, umkumbuke mzazi
Furaha ya mama yangu, ndiyo mimi nilo nayo
Bado mimi nipo shule, safari hini ni ndefu
Karo mama ipo tele, nakuomba Mtukufu
Lijaze hima wimbile, nisome japo marefu
Furaha ya mama yangu, ndiyo mimi nilo nayo
Yakini na taadhima, nitawa mvumilivu
Shule nitaweka hima, chudi ustahimilivu
Kesho nije kusimama, mamangu nami angavu
Furaha ya mama yangu, ndiyo mimi nilo nayo
John Rukono
Thika
Mwanagenzi- Giakanja Boys High School
Similar Posts by The Mt Kenya Times:
- Pupils lead the way at Kitale school’s agriculture field day
- The drought of our own voices: Why Kenya must cultivate literature that mirrors its streets, farms, and hearts and write it in the tongues that know us best
- Beyond acquittal: The Human cost of the Uasin Gishu Education Programme and the search for justice
- Kenya’s debt trap: Who pays the bill?
- Mwea MP Maingi presses government to shield local rice farmers from imports