Wanjohi. P. Mugambi

Alipoondoka baba, mama kuachwa mjane

Ya baba yote akiba, walisema wagawane

Hatukupewa na haba, tuliachwa na ujane

 

Tulisalia kulia, kilio kisicho dawa

Mama akawalilia, huruma akaonewa

Mahali pa kulimia, shamba dogo kukapewa

 

Tulikuwa tu wadogo, yote yakifanyika

Mama na ndugu mdogo, kwenye shamba tukafika

Kulailima mihogo, mahindi na kadhalika

 

Walikujia mazao, siku yetu tukivuna

Wakaipeleka kwao, tukawa chetu hatuna

Yamo kwenye shamba lao,mashangazi wakanena

 

Hima hatukufa moyo , tuliyaishi maishi

Nayo tulokuwa nayo, matumbo ikashibisha

Mama kitutia moyo, yote hayo yangeisha

 

Mkopo alichukua, mama tukaenda shule

Asingelipa hatua, shamba letu lijendele

Nasi ikawa satua, shuleni twende kilele

 

Tulisoma tukilima, huku tukivumilia

Kwa walimu taadhima, sisi tukachikilia

Ilipofika hatima, mosi tukaimbukia

 

Tulipata wafadhiri, tukaenda sekondari

Tukakizika kiburi, masomo tukakariri

Huko tukapata heri, gredi nzuri fahari

 

Chuoni  tulipofuka, kina ami walikuja

Kutuchukua hakika, tuliokuwa pamoja

Tukakatakaa  fika, na vyao vingi vioja

 

Tuliosoma yakini, ndugu akawa daktari

Mimi nami runingani, nikawa mwanahabari

Mama akawa usoni, tabasamu lashamiri

 

Wote waliotuona, midomo walifungua

Walosema tuna la’na, walishindwa kutambua

Wakawa wasemezana, huku wakitwangalia

 

Na sisi tumejifunza, kwa amani tukaishi

Na mama alotutunza, apate nzuri aushi

Daima ni Mungu kwanza, kisha mametu shabashi

 

 

Wanjohi. P. Mugambi

Malenga Kitunguu Machoni

Similar Posts by Mt Kenya Times:

By Wanjohi P. Mugambi

Wanjohi. P. Mugambi

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *