Dr. Wanjohi. P Mugambi
Yaliza mpaka mfu, hali ya humu nchini
Kwa kuwa wale dhaifu, bado wasalia chini
Hata aliye kipofu, aona walo ta’bani
Hali ya humu nchini, yaliza mpaka mfu
Ukiwasikia hofu, yakujaa mtimani
Kiangalia marefu, wapatayo masikini
Ilhali majisifu, wajipa wa uongozini
Hali ya humu nchini, yaliza mpaka mfu
Huahidi maradufu, waingiapo bungeni
Wakakuwa maarufu, wakasahau jamani
Wakala mingi minofu, sambe kwanza hadharani
Hali ya humu nchini, yaliza mpaka mfu
Huwa wasahaulifu, kuwa sote tu ta’bani
Kwa wao uharibifu, tunalia abadani
Lini wata’cha machafu, heri wakatuauni?
Hali ya humu nchini, yaliza mpaka mfu
Yaliza mpaka mfu, hali ya humu nchini
Ila twaomba Raufu, atukinge maishani
Akatupe taarifu, tunapoenda debeni
Hali ya humu nchini, yaliza mpaka mfu
Dr. Wanjohi. PΒ Mugambi
Malenga Kitunguu Machoni
Similar Posts by The Mt Kenya Times:
- Mt Kenya Times ePAPER June 29, 2026
- The KSh12 billion shakedown: How Kenya’s vehicle inspection scheme became a political firestorm
- Eustaquio’s 90+2 stunner sends Canada into last 16 as South Africa fall
- The myth of green pastures in the city
- Zimbabwe’s luxury economy: why wealth without work is not enough