Brian Oigara
Nisije kwenye mazishi, nikalia kikwikwikwi,
Nikijifanya mbishi,lawama ni kwa ukukwi,
Wetu mterehemeshi,aki ya Mungu hazikwi,
Pepa Lobawoi pepa, maua yako nakupa.
Nisije nikajifanya,kuwa mwingi wa subira,
Kivyovyote kujikanya, ningoje mambo kubura,
Mashabiki ukisanya, ndiposa nikupe kura,
Pepa Lobawoi pepa, maua yako nakupa.
Chema nakiitwe chema, watu wote wasikie,
Wewe ni rafiki mwema,naomba nikisifie,
Mola akupee neema, ya kheri akujalie,
Pepa Lobawoi pepa, maua yako nakupa.
Tungetamani dunia, yenye watu kama wewe,
Watu wasio udhia, wanyofu waso kiwewe,
Kwa kweli tungetulia, na kupendana wenyewe,
Pepa Lobawoi pepa, maua yako nakupa.
Mwisho wangu ndio huu, bingwa uzidi kutamba,
Ufike na huko juu,ntini upawe namba,
Magazeti yanukuu, hoja zako ukiamba,
Pepa Lobawoi pepa,maua yako nakupa.
Brian Oigara
Malenga Mla Leo
Similar Posts by The Mt Kenya Times:
- Mt Kenya Times ePAPER July 22, 2026
- DCP green coats flood Parliament after Ol Kalou victory
- Full university sponsorship for 2026: Bold promise or dream deferred?
- Gachagua and Wanjigi deepen opposition talks as Mount Kenya political realignment gathers pace
- Goonland: The shattered ambitions of Kenya’s disposable sons
Kazi aula hii Be. Wanjohi. Napendezwa na Gazeti hili kwa kunyanyua vipaji.