Joseph Abuko
Afrika bara zuri, tuna vingi vyapendeza,
Tunavipaji vizuri, vyenyewe vyajitangaza,
Michezoni tu pazuri, na kandanda tunacheza,
Afrika tunavingi, vizuri twajivunia.
Madini tumejaliwa, dhahabu na almasi,
Hakika tulizaliwa, kwenye Bara zuri sisi,
Afrika mambo sawa, tunalindwa na polisi,
Afrika tunavingi, vizuri twajivunia.
Tuna miti tofauti, kweli madhari mazuri,
Miti inaunda kiti, chapendeza ni kizuri,
Na wanetu mabanati, wanapendeza wazuri,
Afrika tunavingi, vizuri twajivunia.
Tunapenda tamaduni, kuanzia kwa mavazi,
Tunavalia vipini, urembo wetu u wazi,
Na tunalima shambani, sisi ni wachapakazi,
Afrika tunavingi, vizuri twajivunia.
Na tamati nimefika, tuipende Afrika,
Ni Bara nzuri hakika, bara lenye uhakika,
Na Vyakula vya kupika, vipo vipo Afrika,
Afrika tunavingi, vizuri twajivunia.
Mtunzi: Joseph Abuko
(Chuo Cha ICS Nakuru)