DR Congo
Limeniliza nalia, linalofanyika Congo
Mwanadamu nasilia, na wingi tena msongo
Utu umeshasilia, jina lao songombingo
Naililia Congo
Nitazamapo runinga, mambo huko yanaliza
Japo Kenya yatuganga, huko kwataka mu’jiza
Hata watoto wachanga, vita havijawasaza
Naililia Congo
Alipotuumba Mungu, duniani kutuweka
Alitaka walimwengu, kwa amani kujengeka
Ila watu ni miungu, wengi wamebadilika
Naililia Congo
Wanjohi napiga dua, nikiililia Congo
Naiombea afua, ikaone bila tongo
Kilio wanacholia, Mungu waone Wakongo
Naililia Congo
Nikiomba E Rabuka, ikumbuke pia Kenya
Congo kusikokalika, Kenya nako kunasinya
Ni vifo vyaongezeka, uhai vinavyonyonya
Naililia Congo
Dr. Wanjohi. P. Mugambi
Malenga Kitunguu Machoni
Similar Posts by The Mt Kenya Times:
- Mt Kenya Times ePAPER August 29-30, 2026
- Old Mutual swings to KSh882M profit as insurance arm ends losing run
- US pumps KSh930M into Kenya police modernisation
- Kalonzo comes to the Coast with a simple, devastating message: You have been betrayed
- Tear gas, shuttered shops and a government out of touch: The KRA tax revolt that could define Kenya’s road to 2027