Wanjohi. P. Mugambi
Moyo wangu ni hafifu, haya ninapoyanena
Una mengi masumbufu, jinsi yalivyo bayana
Unatariki mapafu, kiyawaza kwa mapana
Wawaza mambo ya penzi,ย penzi lilousaliti
Ulipendwa kiukweli, kama hungependa tena
Ungafunguka asali, ikawa ndo mlo sana
Ila umeonja ukali, nayo makali wavuna
Wawaza mambo ya penzi,ย penzi lilousaliti
Ni mnyonge huu moyo, yakini nguvu hauna
Na yote uyawazayo, majibu yake hauna
Kwa penzi lenye uchoyo, wavunja damu kwa kina
Wawaza mambo ya penzi,ย penzi lilousaliti
Unatamani ya wafu, duniani waso nena
Kwani heri kuwa mfu, ya duniani mepona
Kuliko ya ubarafu, penzini unaovuna
Wawaza mambo ya penzi,ย penzi liloisaliti
Mtima unasumbuka, kwa marefu na mapana
Unatamani hakika, na dunia kuachana
Uchunguni ukatoka, tulio lenye maana
Wawaza mambo ya penzi,ย penzi lilousaliti
Wanjohi. P. Mugambi
Malenga Kitunguu Machoni
Nairobi Kenya
Similar Posts by The Mt Kenya Times:
- Written in gold, wielded in iron: Katiba@16 and the realities of power
- Mang’eni challenges universities to put entrepreneurship at the heart of learning
- Why Jetour struggles to build a fan base in Kenya
- Spleng School Ruiru students enjoy an exciting educational trip to Malindi
- The three-legged stool is wobbling