Leo ninasema wazi,yaliyo moyoni mwangu
Visanga vy siku hizi,vinatikisa rohongu
Vimekua kama jonzi,naapa mbele ya mungu
Vitoto hivi vya Leo ,vinayo maradhi Gani?
Zama zetu Nakumbuka,tulipokua sikuli
Tukionywa twaonyeka,ghulamu na wanawali
Adabu tulishika ,ikapenya Kwa miili
Vitoto hivi vya Leo,vinayo maradhi Gani?
Tuliheshimu wazazi,vile vile majirani
Kutii tulimaizi,ni dhahabu aushini
Tulikemea ajizi,kiamboni na darasani
Vitoto hivi vya Leo,vinayo maradhi Gani?
Mabinti wa siku zile,walijua kutulia
Wangenyoshewa kidole,machozi wangeyatoa
Waliustawi ukale,wachumba kujipatia
Vitoto hivi vya Leo,vinayo maradhi Gani?
Oneni hivi vya Leo,vyajiita vidijito
Vyaishia Kwa nyingi ndweo,duniani na kindoto
Havitunzi Mili Yao,ilozidiwa na joto
Vitoto hivi vya Leo,vinayo maradhi Gani?
Vyatembea vikiringa,ety wao mashangingi
Hata havifungi kanga,mapaja marangirangi
Ukifumbua maninga,taona vyavuta bangi
Vitoto hivi vya Leo,vinayo maradhi Gani?
Vyapenda kuhanja hanja,kujifanyia wasomaji
Midomo vyakunjakunja,magalacha usagaji
Usipokuwa mjanja,vitakutosa Kwa maji
Vitoto hivi vya Leo, vinayo maradhi Gani?
Vyachukia ushauri ,mashikio Yana pamba
Vimejaa ushauri,jinsi vinavyojigamba
Vyazurura kijasiri,usiku sawa na mamba
Vitoto hivi vya Leo,vinayo maradhi Gani?
Havijali maisha ,chochote vyaparamia
Visipojirekebisha,wallahi vitajutia
Malenga vimenichosha,moliwa naviachia
Vitoto hivi vya Leo,vinayo maradhi Gani?
Ukingoni nmefika,chini napiga magoti
Machozi yanitoka,nikipanga mikakati
Wapendwa twahitajika,tukiokoe kizati
Vitoto hivi vya Leo,vinayo maradhi Gani?
Malenga:Winjoy Gacheri
Lakabu: mtoto wa Meru
Chuo kikuu Cha MKU

